Video:Udm Party cracks deepen
Mwanya kwenye chama cha udm uliendelea kupanuka hii leo baada ya katibu mkuu wa chama, martin ole kamwaro na mwenyekiti wa kitaifa, joseph chirchir kuandaa mikutano miwili tofauti ya baraza kuu la chama. Mrengo wa chirchir umepanga kuanza uchaguzi wa mashinani kwa wanachama kuanzia februari saba mwaka huu kabla ya kuandaa uchaguzi wa kitaifa tarehe 22 februari. Aidha, kundi la ole kamwaro linashikilia kuwa mkutano wake ndio halali na maafikio yeyote chini ya kundi la chirchir hayatazingatiwa na wanachama kwa vile yamekiuka katiba ya chama. Patrick amimo ametuandalia taarifa ifuatayo kuhusu mgogoro huo wa udm.